Monday, October 31, 2011

Chanjo Tour;

Rushwa ni kama giza lililotanda kwenye fikra na mioyo yetu. Maeneo mengi ya vijijini hakuna huduma ya Umeme, Kibatari (Koroboi) hutumika kulifukuza giza na kuleta nuru na mwangaza. Ujio wetu kijijini Msoma ulipokelewa na Koroboi ikimulika eneo lote kama taa itoayo nuru na ishara ya kuleta tumaini mahali penye giza nene. Safari ya Chanjo nchini kote imeanzia hapa, kwa mwanga mdogo uangazao mahali pote.

No comments:

Post a Comment