Wednesday, December 28, 2011

CHANJO ILIVYOKONGA WANANCHI MIKOANI


 1. Mwitongo-Butiama nyumbani kwa Mwl.Nyerere, Hili ni jiwe ambalo Mwenge mkubwa huwasha hapo kila mwaka. Vitali Maembe akionesha ishara ya mafanikio juu ya jiwe la Mwenge, alisema ni baraka kubwa kufika hapo yeye na timu nzima ya Chanjo ya Rushwa, iliwachukuwa muda mrefu na nguvu nyingi kufika hapo, vikwazo  vingi vilitokea lakini hawakukata tamaa. chanjo inaendelea

 2. Maswali na majibu kuhusu Chanjo
3. Wengine wanashangazwa na aina hii ya ujumbe na mtindo wa uwakilishaji, watu wa njoro Moshi wanauliza kutaka kujua kwanini Chanjo imekuja kwao na kwanini imeletwa na The Spirits na sio Serikali.
 4. Wengine hawakupenda kusogelea lakini kwa umbali waliokaa walisema wameipata vizuri.
 5. Wakaazi wa kijiji cha Butiama wakisikiliza kwa makini huduma ya Chanjo iliyotolewa kwao na wanamuziki wa The Spirits

6. Wanawake wa Pangani mkoani Tanga wakivunja ukimya juu ya mateso wanayoyapata kama wanawake pale Rushwa inapopewa nafasi hasa katika huduma za kijamii.
7. Vitali Maembe na Wananchi wa Sakura wakijadiliana kuhusu Rushwa 

 8. Watoto waliguswa sana na Chanjo lakini kwa namna ambayo tunaweza tusiijue, inawezekana sana wakawa wameguswa na kuvutwa na mlio mkubwa wa muziki na utamu wa mapigo yake, kilichotokea ni kwamba walihudhuria, walicheza na kufurahi, Chanjo ilikuwa na umuhimu wa aina yao kwao. Walipata Chanjo.
 9. Hapa ilikuwa Njoro, mkoani Kilimanjaro, walipata chanjo na kufurahia lakini ujumbe wa namna hii uliwashangaza
 10. Siku hii watu walinogewa na kusema 'Chanjo imetuvuta wengi nasi tunatamani kutoa Chanjo'

 11. Wakaazi wa Pangani wakihudhuria onesho la Chanjo, hili lilikuwa onesho maalum baada ya watu kuomba tena kupewa chanjo kwa mara ya pili siku ya kwanza haikuwatosha.
 12. Watoto kwa wakubwa wakipata Chanjo Kituo cha mabasi wilaya ya Pangani mkoani Tanga
 13. Wananchi waliutumia vema ujio wa Chanjo, walisema kila kigumu kilicholetwa na Rushwa
14.  Safari Chanjo ilihudhuriwa na Wakinamama na wanawake wengi, lakini wachache sana walizungumza na kuuliza maswali wakati wa majadiliano, wengi walisikiliza na kutafakari wenyewe mioyoni mwao, na baadaye walijadiliana wao kwa wao. Inawezekana kabisa kuwa malezi na tamaduni na taratibu zetu zinachangia haya. Chanjo inaendelea na mchango wao tunauona.

 15. Chanjo wakati mwingine ilikuwa ni kama kitu cha kushangaza, lakini kimewavutia.
16. Watoto waliguswa sana na Chanjolakini kwa namna ambayo tunaweza tusiijue, inawezekana sana wakawa wameguswa na kuvutwa na mlio mkubwa wa muziki na utamu wa mapigo yake, kilichotokea ni kwamba walihudhuria, walicheza na kufurahi, Chanjo ilikuwa na umuhimu wa aina yao kwao. Walipata Chanjo.
 17. Salumu Mpute akicharaza Bass huku akisikilizwa na watu kwa makini wakati Spirits ikitoa chanjo.
18. Watoto waliguswa sana na Chanjolakini kwa namna ambayo tunaweza tusiijue, inawezekana sana wakawa wameguswa na kuvutwa na mlio mkubwa wa muziki na utamu wa mapigo yake, kilichotokea ni kwamba walihudhuria, walicheza na kufurahi, Chanjo ilikuwa na umuhimu wa aina yao kwao. Walipata Chanjo.
19. Wananchi walikula kiapo baada ya kupata Chanjo, Kiapo hufanyika mara mbili mwanzo wa onesho na baada ya majadiliano, hiki huwa ni kipimo bora cha kujua kama watu wameelewa.
20. Safari Chanjo ilihudhuriwa na Wakinamama na wanawake wengi, lakini wachache sana walizungumza na kuuliza maswali wakati wa majadiliano, wengi walisikiliza na kutafakari wenyewe mioyoni mwao, na baadaye walijadiliana wao kwa wao. Inawezekana kabisa kuwa malezi na tamaduni na taratibu zetu zinachangia haya. Chanjo inaendelea na mchango wao tunauona.

21. Bw. Makame akifafanua ukimya wa watu 'Watu wanashindwa kusema lakini wanaumia, watu wanapatashida kwenye kupata kazi na nafasi katika mashamba ya Mkonge huku Sakura na sehemu nyingine hapa Tanga, lakini wanaogopa kusema au kulalamika kwakua mkiondoka hapa watanyanyasika kwakuwa wamesema ukweli'
22. Siku ya mkesha wa Uhuru, watu waliokusanyika katika kiwanja cha michezo cha Babati mkoa wa Manyara walipata fursa ya kupewa Chanjo. Waliipokea na kushiriki vema.
23. Baadhi ya watalii walioitembelea Tanzania walipata bahati ya kupata Chanjo. Walishiriki na wenyeji jukwaa moja.
24. Timu ya Chanjo ilipofika Butiama ilimtembelea Chifu wa sasa wa wazanaki, Mzee Wanzagi aliwakaribisha vizuri na kuwaelezea jinsi Mwl. Nyerere alivyoipenda nchi yake na kuichukia Rushwa.
25. RUSHWA NA EWURA, Mafuta machafu na yenye maji mengi kutoka katika vituo vya mafuta vilivyothibitishwa. Wanamuziki wa Chanjo wakishusha Tenki la mafuta la gari kumwaga mafuta, iliwalazimu kufanya hivyo zaidi ya mara tatu katika safari. na kutembea mwendo mrefu kwa miguu na pikipiki kutafuta mafuta ya 'videbe' yaliyo salama ili kuendelea na Safari.


Monday, November 14, 2011

..MAPAMBANO KUPINGA MAPAMBANO!!


"Tarehe 10 Nov 2011 Nilishushwa jukwaani na Askari polisi, maeneo ya Parking wilayani Nzega mkoani Tabora, walinishikilia kwa saa nzima na kunikabidhi kwa maafisa wa TAKUKURU-PCCB wilaya. waliniachia baada ya masaa manne, kwa vitisho vya kufuta usajili wa bendi yetu, kunipiga marufuku kuimba kuhusu Rushwa Tanzania na kunifutia kibali changu cha kufanya kazi za sanaa. Mungu ibariki Tanzania."- Vitali Maembe.

CHANJO TOUR INTERRUPTED!!


As from when it commenced on the 19th October 2011, Chanjo has already covered 7 regions: Rukwa,  Mbeya, Iringa, Morogoro, Dodoma, Singida and Tabora.  In this coverage a total of 23 performances and at least 7,840 people who have attended.

Fortunately, they all responded well by being attentive and they were free to participate. Some explained how they understand corruption, its forms and courses while some even gave vivid examples of cases in their daily life. However there are few who seemed to suggest that we can not do without corruption.

Another challenge is that the PCCB interrupted the program on the 10th Novermber 2011. While at the performance in a parking area, in Nzega Tabora region showed up two police officers in casual clothes. They ordered Vitali Maembe to leave the stage and to get in the police vehicle and they headed to the district police station.

At the station they told him to wait for the PCCB  officer for about an hour. During that hour the police officers were interrogating him without writing anything. When the PCCB officer arrived, Vitali was handed over to him.





From around 1800 Hrs to 2200 Hrs the three officers mocked all the efforts put in this tour. They claimed to have the authority to stop Vitali from singing about corruption. Then, they could denounce the band registration, and they would also stop the permits for the tour. They also decleared that, at the end of the tour, Vitali would end up being the loser.  Their claims were that he had insulted the PCCB.
Meanwhile they were communicating on the phone with the District Commissioner, Head of the District Police Station and someone from the national Security council. After hours of interrogation they let him go. 

Now the whole band of  The spirits is in Bagamoyo, soon at the end of this week they will carry on with the tour.

Briefly, this is what has been happening over the last month, we will keep you posted. 

Vitalis M. Maembe.
Asante.

Friday, November 4, 2011

..KAMPENI YA CHANJO INAZIDI KUSONGA MBELE

Dodoma Mwl. Nyerere Square chanjo ilitolewa hapo.

"karibuni sana mtoe chanjo ya rushwa"

"kijijini Mpui chanjo imefika"

Pokeeni chanjo mkawaambie na wengine 'rushwa ni adui wa haki na maendeleo'.

'nimewachagulia huyu, awe Tambiko la chanjo'

Ahsante sana!

Hapa ndipo alipozaliwa Vitali Maembe miaka 35 ilopita kijini Mwazye, chanjo imefika hapa

Habari za asubuhi?
Onyesho la Kwanza kijijini Msoma,Ilikuwa siku ya Jumapili baada ya Ibada, wanakijiji waliudhuria kwa wingi kupata Chanjo dhidi ya Rushwa, Uvivu na Ubinafsi.

Taa hii ilitoa nuru na mwanga kwa usiku wote wa siku a kwanza kuwasili kijijini Msoma, nuru yake ilifanikisha kufanyika kwa Tambiko la kuomba na kubariki safari  na Kazi nzima ya Chanjo dhidi ya Rushwa, Uvivu na Ubinafsi.

 

       Kwa mila nyingi za kiafrika mgeni hukirimiwa kwa kinywaji kama ishara ya upendo na ukarimu. Kijijini Msoma timu ya Chanjo ilikaribishwa kwa kinywaji cha Asili ‘KOMONI’ kama sehemu ya ukarimu na pia kama sehemu ya Tambiko komoni ilitumika kama mbadala wa Chimpumu pombe ya asili ya eneo hilo, hii ilikuwa kuwakaribisha wageni na kuwaombea heri katika safari ndefu ya mapambano dhidi ya Rushwa.


4.     Sehemu ya umati wa watu waliohudhuria Chanjo dhidi ya Rushwa, Uvivu na Ubinafsi kijijini Msoma, Sumbawanga Vijijini.



 Mmoja wa watu waliovutiwa na Muziki pamoja na Ujumbe unaoelimisha kuhusu Rushwa Kijijini Mwazye, Sumbawanga vijijini, hii ilikuwa ni sehemu ya onyesho la Chanjo dhidi ya Rushwa, Uvivu na Ubinafsi.


 Japokuwa alikuwa na hamu kubwa ya kusikiliza muziki, lakini ‘kucheza muziki’ ni jambo ambalo watu wengi wa maeneo ya vijijini hukosa fursa hiyo, kuwepo kwa onyesho la Chanjo kuliwapa fursa wanakijiji wa Mwazye kuelimika kuhusu Rushwa na kupata wasaa wa kuburudika na Muziki pia.
                                             Watu waliohudhuria onyesho la Chanjo kijijini Mwazye.


Vitali Maembe akitoa Chanjo dhidi ya Rushwa, Uvivu na Ubinafsi kwa wanakijiji waliohudhuria Onyesho hilo kijijini Mwazye.

Sehemu kubwa ya zoezi zima la safari ya Chanjo ya Rushwa ni kujenga jukwaa la majadiliano linalowezesha wanaharakati wa Chanjo kuweza kufanya majadiliano ya wazi kuhusu Rushwa na matatizo yanayoletwa nayo. Msanii Vitali Maembe akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa majadiliano, Kijijini Mwazye.





Kucheza kwa furaha huku ukitoa ujumbe kuhusu Rushwa kunashawishi Umma kuamini kuwa Rushwa si Mwiko kuijadili, njia mbali mbali zinaweza kutumika kuweza kufikisha ujumbe mojawapo ikiwa sanaa asilia.Vitali Maembe akicheza mojawapo ya ngoma za asili, Sumbawanga.


1.    Kuimba pamoja na hadhira wimbo unaofahamika zaidi kunajenga hamasa ya kushiriki katika majadiliano, zoezi mojawapo kubwa katika safari ya Chanjo ni kuishawishi hadhira kuwa mapambano dhidi ya Rushwa hutakiwa kufanyika katika Umoja wetu. Msanii Vitali Maembe akiimba pamoja na hadhira mojawapo ya nyimbo maarufu kijijini Mwazye.